Serikali yakanusha kujiondoa itifaki mahakama ya afrika ya haki za binaadam

 Na Seif Mangwangi,Arusha

Serikali ya Tanzania imesema haijajiondoa kwenye mahakama ya Afrika ya watu na Haki za Binaadam (AfCHPR), kama inavyoelezwa na wadau mbalimbali.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amesema ilichofanya Tanzania ni kujiondoa kwenye ibada ya 34(6), ya mkataba wa mahakama hiyo.

Ibara ya 34(6), ya mkataba wa Mahakama hiyo inaruhusu watu binafsi na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kuwa na haki ya kufikisha moja kwa moja kesi za ukiukwaji wa haki za binaadam katika mahakama hiyo dhidi ya Serikali.

Naibu Waziri Mbarouk amesema Serikali ya Tanzania imejiondoa kwenye ibara hiyo kwa kuwa Tanzania bado ina njia vyombo vingi vya kusikiliza mashauri ya uvunjwaji wa Haki za binaadam na kutoa maamuzi.

Uamuzi huo ulifikiwa kufuatia mashauriano na majadiliano ya kina kwa manufaa ya nchi na sio ya kisiasa,” naibu waziri huyo alifafanua katika Mahojiano ya Pamoja ya Mahakama ya Afrika na Kamati ya Wawakilishi wa Kudumu ya Umoja wa Afrika AU, yaliyoanza jana jijini Arusha .

“Maamuzi ya kujiondoa kwenye mkataba dhidi ya ibara hiyo yalifanyika baada ya mashauriano ya kina kuhusu maamuzi binafsi ya nchi na sio hamasa ya kisiasa,” Amesema Naibu Waziri Mbarouk katika kikao cha pamoja kati ya mahakama ya Afrika na kamati ya kudumu ya Umoja wa Afrika 

Balozi Mbarouk alisisitiza dhamira ya Tanzania kuendelea kuheshimu maamuzi ya  mahakama  

na  kuzingatia kanuni za haki za binadamu.

“Tanzania ilikuwa inasubiri kwa hamu na kwa dhati kuanzishwa kwa mahakama hii kama ilivyo kwa taasisi zingine za kimahakama ambazo zina makao yake makuu hapa nchini… kwa hiyo tunafurahia uhusiano wa kikazi kati ya Serikali na AfCHPR,” alisema

Naibu Waziri hata aliitaka  mahakama hiyo yenye makao yake makuu Jijini  Arusha kuweka viwango vinavyoendana na hali halisi kwa kuzingatia muktadha wa Afrika na mamlaka ya nchi.

Alisema kuna umuhimu wa mahakama hiyo kuheshimu sheria za nchi wanachama wa mahakama hiyo na kusema baadhi ya maamuzi  yamekuwa yakikiuka sheria za nchi na ndio sababu baadhi ya nchi zinaamua kujiondoa.

Kauli ya Balozi Mbarouk inakuja wiki moja baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuihakikishia mahakama ya Afrika  AfCHPR uungwaji mkono kamili wa serikali. 

Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Tanzania ilikuwa muumini thabiti wa masuala ya haki za binadamu kama vile utawala wa sheria na haki, kama sharti la maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Ibara ya 34(6) ya Itifaki ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Kibinadamu na Watu inayoanzisha Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu inazitaka Nchi Wanachama wa Itifaki hiyo kutoa tamko tofauti ili kuruhusu ufikiaji wa moja kwa moja kwa watu binafsi nna mashirika ya serikali kuleta kesi dhidi yao katika Mahakama ya Haki za Kibinadamu ya Afrika. Tanzania, ambayo iliweka tamko lake Machi 29, 2010, ilitangaza kujiondoa kwa tamko hilo mnamo Novemba 14, 2019.

Tanzania, ambayo iliweka tamko lake Machi 29, 2010, ilitangaza kujiondoa kwa tamko hilo mnamo Novemba 14, 2019. 

Nchi nyingine ambazo zimejiondoa katika tamko hilo lakini bado zimesalia kuwa watia saini wa Mahakama hiyo ni pamoja na Rwanda, Ivory Coast na Benin.

Hapo awali, Rais wa AfCHPR, Imani Daud Aboud alikiri kwamba shughuli za Mahakama zilikuwa zikipunguzwa na kujiondoa kwa baadhi ya majimbo.

 “Kama kuna lolote, hii inapunguza imani ya Mahakama miongoni mwa Waafrika,” alisisitiza.

 Kwa mujibu wa Rais wa Mahakama hiyo, Mahakama inajitahidi kusisitiza haja ya kuridhia itifaki juu ya uanzishwaji wa mahakama.

“Tumekuwa tukishirikisha nchi mara kwa mara na kufikia sasa tumetembelea nchi 19 ambazo bado hazijaidhinisha Itifaki,” alisema.

Zaidi ya washiriki 100 wakiwemo Majaji wa Mahakama na idara husika za Tume ya Umoja wa Afrika (AU) walitarajiwa kuhudhuria mafunzo  hayo ambayo yanalenga kurejesha hali ya kuaminiana, ushirikiano na kujenga imani.