Uwamakizi ni chuo cha utunzaji mazingira duniani-jenerali mstaafu mwamunyange

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange akizungumza wakati wa ziara ya siku moja ya mafunzo mara baada ya kufika Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja na Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo akizungumza wakati wa ziara hiyo kushoto ni MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange


Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja


MTAALAMU wa Mazingira Tanga Uwasa Ramadhani Nyambuka akieleza jambo wakati wa ziara hiyo kulia ni Meneja Ufundi wa Tanga Uwasa Mhandisi Rashid Shabani

Sehemu ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) wakifuatilia maelezo kuhusu namna ya uhifadhi wa mazingira kutoka kwa Mtaalamu wa Mazingira Tanga Uwasa Ramadhani Nyambuka


Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly katikati akisisitiza jambo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange kushoto wakati wa ziara hiyo kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja wa kwanza kushoto ni
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly wakati wa ziara hiyo wa pili kutoka kulia aliyevaa shati jeupe ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo

Mwenyekiti wa Kikundi cha Uwamakizi wilayani Muheza Twaha Rajabu kushoto akieleza namna wanavyotunza mazingira katika vyanzo vya maji kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya Dawasa wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange


Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly kushoto akiteta jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja wakati wa ziara hiyo
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange akitoka kwenye maeneo ya uhifadhi ya Uwamakizi wakati wa ziara hiyo
Maji yakitiririka kutoka kwenye bwawa la mabayani
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange katika akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa bodi hiyo wakati walipotembelea bwawa la mabayani wakati wa ziara ya siku moja ya mafunzo Jijini Tanga kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa
Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Dar es Salaam (Dawasa)
Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange ameridhishwa na shughuli
zinazofanywa na umoja wa wakulima wahifadhi wa Mazingira Kihuwi
(Uwamakizi) huku akieleza hicho ndio chuo kikuu cha utunzaji wa
mazingira sio kwa Tanzania  bali Afrika na hata Dunia.
Huku
akiwataka watu waje kuona namna hatua wanazozichukua kuweza kutunza
vyanzo vya maji uhifadhi mazingira ambao umekuwa na tija kubwa kwa
kushirikishi wananchi ambao wamekuwa wakiishi karibu na maeneo
yaliyokuwa na vyanzo hivyo.
Mwamunyange
aliyasema hayo juzi wakati wa ziara yao ya kimafunzo ya siku moja
iliyoandaliwa na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tanga (Tanga
Uwasa) ambapo walitembela maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la Bustani ya
Uwamakizi katika mlima wa mfano wa shughuli za uwamalikizi,
Maeneo
mengine ambayo walitembelea ni eneo la uhifadhi wa mto Mihale katika
mpaka unaotenganisha kijiji cha Kimbo na Shembekeza vilivyipo kwenye
kata ya Kisiwani na Potwe wilayani Muheza na Bwawa la kuhifadhi Maji la
Mabayani.
Alisema
wamefurahishwa sana na dhana hiyo ya Uwamakizi kwa sababu ni nzuri kwa
sababu wamegeuza changamoto kuwa fursa nzuri kwa kutumia ubunifu na
kuongeza vitu vipya kwa kuhakikisha wanatunza mazingira
 “Kwa
kweli nimefurahishwa sana na ubunifu huu sikutarajia ningeuona hapa
niwapongeze sana muendelee hivyo na ari na moyo wa ushirikiano
muendeleze upendo na amani maendeleo yetu yanatakiwa kuletwa sisi
wenyewe ”Alisema Mwenyekiti huyo wa Bodi ya Wakurugenzi.
Alisema
walisikia sifa nyingi kuhusu juhudi na kazi nzuri waliyoipata katika
utunzaji mazingira na vyanzo vya maji baada ya kusikia sifa hizo
wakasema ni vuzuri wao kama bodi waje wakajionee wenyewe hizo sifa
zinatokana na nini isije kuwa maneno.
Aidha
alisema hivyo wakawaomba Tanga Uwasa kwa ajili ya bodi kuja kujionea
wenyewee hayo yote na walifika na wakaanza mazungumzo nao baada ya
maelezo wakafika kwenye baadhi ya maeneo kujionea wenyewe huku wakihaidi
kwenda kuwa mabalozi wao.
Awali
akizungumza kabla ya kuanzia ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally Fungo aliwakaribisha huku akieleza
kwamba hiyo ni heshima kubwa kwao na wameona kuna kitu wanakikosa
ambacho watawaonyesha
Aidha
alisema ni madhumni yao ziara kama hizo sio hii ya pekee bali ziweze
kuwa nyingi ili waweze kushirikiana kila fursa itakapojitokeza na kila
wakati itakapohitajika.
“Katika
ziara hii leo watatembelea bwawa la kuhifadhi maji mabayani,kijiji cha
Mashewa kitongiji cha ikulu kuangalia uhifadhi wa kingo za mto na jinsi
uwamakizi wanavyotumia mita 60 za uhifadhi wa mto,kutembelea ofisi za
uwamakizi ,wakaona vikundi vya sanaa cha uhamasishaji uhifadhi wa
mazingira na kuangalia eneo lilioandaliwa”Alisema Dkt Fungo
Naye
kwa upande wake Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly
alisema ziara hiyo ya mafunzo ni kujifunza namna ya utunzaji wa vyanzo
vya maji ndio ambacho kimewafanya kuja kuona.
Akizungumza
wakati wakiwa kwenye bwawa la Maji la Mabayani walielezwa namna
wanavyotumia sheria ya mita 500 kwenye bwawa hilo ambalo linatumika kama
chanzo cha maji.
Hata
hivyo alieleza wana kijiji wanalinda wenyewe hata mtu akiwa anakata mti
hapa anakutwa amezingizwa tayari hatua ambayo ilimfurahisha Mwenyekiti
huyo wa Bodi ya Wakurugenzi ya Dawasa Jenerali Mstaafu Davis
Mwamunyange.