Rais jpm aahirisha sherehe ya mashujaa

Rais John Magufuli ameahirisha sherehe za mashujaa zilizopangwa kufanyika Julia 25 mwaka huu jijini Dodoma .

Taarifa kutoka Ikulu iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu Gerson Msigwa  zinadai kuwa pamoja na kuahirisha sherehe hizo Rais amewataka watanzania kutumia siku hiyo kuwakumbuka na kuwaombea mashujaa wote.