Breaking news : mwenyekiti wa chadema freeman mbowe avamiwa na kushambuliwa


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni  Freeman Mbowe ameshambuliwa na kujeruhiwa na Watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani kwake jijini Dodoma usiku wa kuamkia leo Jumanne Juni 9,2020.



Msemaji wa CHADEMA Tumaini Makene amethibitisha kuwa Mbowe amevamiwa na kushambuliwa na watu wasiojulikana.


“Ni kweli ameshambuliwa na ameumizwa,amepelekwa Hospitali kwa ajili ya matibabu. Tutatoa taarifa zaidi baaadae”,amesema Makene.