Kamwelwe: muda wa kusajili laini za simu hautaongezwa

Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema serikali
haitaongeza muda wa kusajili laini za simu kwa alama za vidole, huku
akitahadharisha kuwa katika siku zilizosalia, kasi ya wizi wa kimtandao
kupitia simu za mkononi imeongezeka.


Amesema
hayo jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu
siku zilizobaki kabla ukomo wa siku 20 alizotoa Rais John Magufuli,
haujawadia. Mwisho wa usajili ni Januari 20 mwaka huu.

“Kumejitokeza
wizi wa kimtandao; wananchi tuwe macho sana tunapomalizia hizi siku
zilizosalia kabla laini ambazo hazijasaliwa hazijazimwa. Watu wanatumia
siku chache zilizosalia kuibia watu kwa kiwango cha juu; bila kuwa
makini, watu tutaibiwa sana,” alihadharisha Waziri Kamwelwe.

Waandishi
wa habari walipotaka kujua kama siku za usajili huo kwa alama za vidole
zitaongezwa, waziri alisema: “Hakuna siku kuongezwa; siku za usajili
hazitaongezwa.”