Nhif yawapiga msasa wanahabari mkoa wa mbeya kuhusu vifurushi vya bima ya afya

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF) Bw. Bernard Konga akiongea na wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya, ambapo aliwasisitiza kuhusu umuhimu wa kutumia vyombo vyao vya habari kuwaeleza wananchi faida za kujiunga na vifurushi vipya kwani vimezingatia makundi yote katika jamii kwa lengo la kuhakikisha kila mtanzania anakuwa na uhakika wa huduma ya matibabu. Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya
Mkurugenzi wa Huduma za Wanachama wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF)Bw. Christopher Mapunda akiongea na wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya, ambapo alisema kuwa viwango katika
vifurushi vya bima ya afya sio gharama za matibabu bali ni uchangiaji ndio maana hata ukiumwa na kutumia zaidi ya kiwango cha laki moja na tisini na mbili, mfuko utagharamikia matitabu hayo. Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya
Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF) Bw. Hipoliti Lello na akitoa mada kwa wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya, ambapo aliwaeleza kuwa mpango wa
vifurushi sio mpya na NHIF imeanzisha mpango huo kwa lengo la kuwafikia watanzania wengi zaidi kulingana na mahitaji yao. Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya.
wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mbeya wakifuatilia uwasilishaji wa mada kutoka kwa wataalam wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF), Tarehe 15.12.2019 Mkoani Mbeya
PICHA NA IDARA YA HABARI-MAELEZO
NA MWANDISHI WETU, MBEYA
 
Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya
(NHIF) Umewapiga Msasa wanahabari Mkoa wa Mbeya kuhusu Vifurushi vya
Bima ya Afya na kuwasisitiza kutumia kalamu zao kuwaeleza wananchi
umuhimu wa kujiunga ili kuwa na uhakika wa matibabu.
Akiongea wakati wa Kikao hicho
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya Bw. Bernard Konga
amewaeleza wanahabari hao kuwa kwa namna ambavyo mfuko umetengeneza
vifurushi umezingatia gharama za matibabu ya kawaida ambayo ukienda
hospitalini lazima uyapate.
“Leo hii wapo wanaopotosha
kuhusu gharama hizi, hatuwezi kuwaacha watanzania ambao wapo tayari
kutumia bima ya afya ili kupata matibabu na kusema tusubiri,
niwahakikishie tumefanya tafiti, kiasi cha Shilingi laki moja na tisini
na mbili kimezingatia gharama za matibabu ya kawaida ambayo ukienda
hospitalini lazima uyapate na utaratibu huu ni niwa hiari”-Alisema Bw.
Konga.
 
Aidha, Bw. Konga alisema kuwa
umefika wakati kwa wananchi kujikatia bima ya afya kabla ya kuugua hasa
katika kipindi hiki ambacho mfuko umeanzisha mpango wa vifurushi ili
kuwa na uhakika wa matibabu na kupuuza maneno ya baadhi ya watu
wanaoendesha mijadala isiyo na tija.
Naye Mkurugenzi wa Huduma za
Wanachama wa Mfuko huo Bw Christopher Mapunda alisema kuwa viwango
katika vifurushi vya bima ya afya sio gharama za matibabu bali ni
uchangiaji tu na ndio maana hata ukiumwa na kutumia zaidi ya kiwango cha
laki moja na tisini na mbili, mfuko utagharamikia matitabu hayo bila
kujali kuwa umetibiwa kwa kiasi gani.
 
Awali akiongea wakati
akiwasilisha mada kwa wanahabari hao Meneja Masoko na Huduma kwa Wateja
wa Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya( NHIF)  Bw. Hipoliti Lello alisema
kuwa mpango wa vifurushi sio mpya na NHIF imeanzisha mpango huo kwa
lengo la kuwafikia watanzania wengi zaidi kulingana na mahitaji yao