Fifa yatangaza viwango vipya vya soka duniani

Shirikisho la soka duniani FIFA limetangaza viwango vipya vya soka duniani huku Belgium wakiendelea kuwa namba 1,

Kwa upande wa Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeendelea kubaki nafasi ya 134 kwenye viwango vya ubora vya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) vya mwezi Oktoba 2020

Uganda imeendelea kuwa kinara kwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ikiwa nafasi ya 76 ikifuatiwa na Kenya iliyo nafasi ya 103

Nchi nyingine zilizo ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na nafasi zao ni Rwanda (133), Ethiopia (146), Burundi (148), Sudan Kusini (168), Djibout (185), Somalia (197) na Eritrea (205)

Kwa Afrika, vinara ni Senegal wakifuatiwa na Tunisia na nyuma yao wapo Algeria wakati wanaoshika nafasi ya nne ni Nigeria na Morocco wako nafasi ya tano

Top 20:

1 Belgium

2 France

3 Brazil

4 England

5 Portugal

6 Spain

7 Uruguay

8 Argentina

9 Croatia

10 Colombia

11 Mexico

12 Italy

13 Denmark

14 Germany

15 Netherlands

16 Switzerland

17 Chile

18 Poland

19 Sweden

20 Wales.