Kamati ya bunge ya pac yatembelea mradi wa maji wa auwsa

*Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Naghenjwa Kaboyoka imetembelea na kukagua utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Arusha na baadhi ya maeneo katika wilaya ya Arumeru. Mradi huo unatekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jiji la Arusha (AUWSA)*