Madiwani arumeru manusura kutoana roho,dc muro aamuru kuhairishwa kwa kikao

Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndg Jerry Muro akitoa tamko la kuhairisha kikao hicho baada ya kuona amani imepotea
Afisa wa Jeshi la polisi akiwaomba viongozi hao wa baraza
kutawanyika baada ya kupokea amri kutoka kwa Mkuu wi laya
madiwani wakianza kunyanyuka na kutoka nje ya ukumbi

Na Lucas Myovela_Arusha.

Mkuu
wa wilaya ya Arumeru Ndg Jerry Muro amelazimika kuamuaru jeshi la
polisi kuwatawanya madiwani na washiriki waliyokuwa ndani ya ukumbu wa
mikutano wa Halmashauri hiyo kwania ya kuepusha vurugu zilizo anzishwa
na madiwani wa halmashauri hiyo.


Awali
myenyekiti wa baraza hilo la madiwani Ndg Wille Njau alisoma ajenda ya
kikao hicho na kutoa muongozo kwa madiwani wengine ili kuchangia ajenda
hizo na kuruhusu maoni na mapendekezo ya madiwani hao.

Vurugu
hizo zilianza ambapo diwani wa kata ya Kikwe Ndg Paul Samweli shango
(CCM)  aliomba muongozo wa kutaka kujua juu ya kuhudhuria kwa diwani wa
kata ya Maluvango Bi Digna John Nassari ilihali mwenyeketi wa halmashuri
hiyo alitangaza kuwa diwani huyo siyo diwani tena kupitia chadema na
amevuliwa uwanachama wake.

Katika
mvutano huo uliyomuhusisha diwani wa kata ya Maluvango (chadema) kwa
100%,juu ya maudhulio yake ya kikao hicho pasipo taarifa ambapo
alitolewa kwa utaratibu na kanuni zao mnamo tarehe 18 May mwaka huu na
leo hii ameudhulia kikao pasipo utaratibu na sheria zao na kanuni kitu
walicho hoji kama baraza hilo nila mtu mmoja au wawili.

“Mh
mwenyekekiti hatuwezi kuendelea na baraza kwasasa mpaka utakapo tuambia
kwanini Mh Digna ameudhulia kikao pasipo utaratibu wala kutueleza
madiwani wenzake na ulimuondoa mwenyewe kwa utaratibu na ukatangaza
kwamba amevuliwa uananchama wa chama chenu leo hii hautaki kutueleza
kwahili halivumiliki hata aje nani hapa hakuna kikao mpaka utakapo weka
wazi” alisema diwani mmoja wa ccm.

Takribani
dakika 100 za mabishano kati ya madiwani na mwenyekiti wa  Halmashauri
ya Meru hazikuweza kuzaa matunda ya maelewano na kuchukua sura mpya
baina ya madiwani wa ccm kusimama kupinga uendeshwaji mbuvu na
wakiholela kwa baraza hilo na kuungwa mkono na madiwani wa chadema ambao
pia hawana imani na mwenyekiti wao licha kutokana na chama chao.

Mara
baada ya mvutano mrefu ndipo busara za Dc Murro zikafuata za kuamuru
kuhairishwa kwa baraza hilo hadi pale watakapo kaachini na kuelewana na
kumtaka mwenyekiyi huyo awe na busara ya kiuongozi maana wote
wanawawakilisha wananchi waliyo wachagua na kumtaka ajitathimi juu ya
mwenendo wake wa uongozi kama mwenyekiti wa Baraza.

“Mwenyekiti
toka nimekaa hapa hakuna hoja yeyeote iliyosikilizwa zaidi ya
marumbanao na madiwani wako wote kusimama kwa nia ya kutokuwa na imani
na wewe na wewe hutaki kuwaweka sawa ili muelewane sasa nilihairisha
baraza hili kwa maana naona amani imesha vurugika na kama mwenyekiti wa
ulinzi na usalama wilaya ya Arumeru kuanzia sasa watu wote mtoke nje
nimelihalisha baraza msije pigana mbele yangu kama mnamambo yenu huko
huko nje siyo hapa hapa tumekuja kutatua kero za wananchi”. Alisema Dc
muro.

MTITI WA NJE YA BARAZA BAADA YA DC KUCHOMOA BETRI.

Kwa
upande wake diwani aliyevuliwa uanachama anaeleza kwamba Mwenekiti wa
baraza hilo alisha andikiwa barua na katibu mkuu wa chama cha demokrasia
na maendeleo chadema Bw Vicent Mashinji mnamo tarehe 28 May 2019 na
kwaelekeza viongozi wa chadema kumrudishia unachama wake diwani huyo
pamoja na cheo chake mara moja kwa kile alicho andika kuwa
hawakuzingatia kwa kutokufuata utaratibu.

“Nilitolewa
ndani ya baraza tarehe 18 May 2019 nikatoka salama na tarehe 25 May
mwaka huu nikakata rufaa ili kupinga kuvuliwa uanachama wangu pasipo
kujua kosa halali ni lipi na kwa bahati nzuri tarehe 28 nikajibiwa na
katibu mkuu wa chadema lakini sasa cha kushangaza mwenyekiti wetu wa
baraza hataki kuwatangazia madiwani wenzangu kwamba nimeshinda na
nimerudi katika nafasi yangu hii siyo haki maana siku ananitoa nje
nilidhalilika sana lakini nilikubali na kumtanguliza mungu wangu mbele
kwanini leo hataki kukiri mbele ya Baraza hili kuwa mimi ni diwani
halali na wanilipe stahiki zangu zote walizo zizuia hapo awali za toka
mwezi wa nne mwaka huu”. Alisema Digna Nassari.

Ikumbukwe
tu baraza hilo kwasasa linaingia katika sura mpya baada ya madiwani
waliyo kuwa wa chadema na kuhamia chama cha mapinduzi ccm kwa kile
kilichodaiwa ni kumuunga mkono Rais Johm Magufuli katika utendaji wake
makini na madiwani hao kuwa na nguvu kibwa ya kutetea wananchi wao
waliyo wachagua.