Madiwani tunduru watakiwa kushiriki malezi na makuzi ya watoto

Afisa maendeleo ya jamii Mariam Juma akikabidhi kitabu cha malezi na makuzi Mkurugenzi mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Tunduru  Chiza Marando wakati wa uzinduzi wa program ya Malezi na makuzi ya Mtoto  ngazi ya Halmashauri.

 Na Joyce Joliga 

Tunduru.

Madiwani wa Halmashauri  ya wilaya ya Tunduru, wametakiwa kushiriki kwenye zoezi la  utoaji wa elimu ya kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu na kusimamia malezi na makuzi  ya watoto wenye mri wa miaka 0-8  hasa kipindi cha ukuaji ili kuwa na  taifa bora na kusaidia watoto kupata elimu na kutimiza ndoto zao.

Hayo yamesemwa na Ofisa maendeleo  ya jamii mkoa Mariam Juma  wakati  akitambulisha  program ya Malezi  na makuzi ya Mtoto kwa Madiwani wa Halmashauri  hiyo  kwa niaba ya Ofisa Ustawi wa jamii wa mkoa wa Ruvuma Victor  Nyenza. 

Program ya malezi  na makuzi  na maendeleo ya Mtoto  imetambulishwa jana kwa Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru katika kikao Cha Baraza la kawaida la robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/3015 kilichofanyika katika ukumbi wa klasta ya walimu wa taarifa ya mlingoti mjini .

Mariam  alisema , serikali imeagiza jamii kuwekeza zaidi kwenye malezi bora kwa watoto chini ya miaka 0 hadi 8 kipindi ambacho ubongo wa mtoto hukua kwa asilimia 100 na kuwa muongozo wa maisha yake yote 

Aidha,Madiwani wametakiwa kuiingiza  program hiyo kwenye mipango yao ya  Halmashsuri kwa kuungiza kwenye bajeti zao ili utekelezaji wake uweendelevu.

Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru  mkoani Ruvuma wakifatilia uzinduzi wa program ya malezi na makuzi ya Mtoto wakati wa kikao cha baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo .

Alisema  program hiyo inatekelezwa katika kipindi Cha miaka mitano ambayo ilianzia mwaka 2021/2022 , 2022/2023,2023/2024 na itaishia 2024/2025.

Alisema ingawa matokeo ya mpango huo hayawezi kuonekana kwa haraka lakini juhudi zake zinalenga kuwalea watoto  kwa kufuatia misingi imara ya maisha Bora kwa kuwa na faida kubwa kwa taifa .

Alisema katika utekelezaji huo serikali imewaelekeza maafisa ustawi wa jamii , maafisa kutoka Idara ya maendeleo ya jamii maafisa wa madawati ya jinsia pamoja na NGOs kushiriki kwenye  utowaji wa elimu hiyo. 

Akizungumzia program hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Haillu Hemedi Mussa  alisema kuwa taarifa hizo zimefika kwa wakati na  kwamba Halmashauri yake imeipokea kwa mikono miwili na akaahidi kuifanyia kazi 

Alisema program  hiyo kwa wilaya ya Tunduru ni muhimu kutokana na wilaya yake kuwa nyuma kwa elimu na kwamba ufuatiliaji wa malezi hayo utawasaidia wananchi kuwa na watoto Bora .

Naye Benaya Wilishangi, anawataka madiwani kusikiliza wataalam wa mezi na  makuzi ili kujenga jamii yenye ustawi bora ikiwa ni pamoja na kuondokanana  udumavu kwa watoto  chini ya miaka mitano.