Majimbo manne ya uchaguzi zanzibar yafutwa

Tume ya Uchaguzi Zanzibar imefuta majimbo manne ya uchaguzi Zanzibar na kubakiza majimbo 50 badala ya majimbo 54 yaliokuwepo awali.

Jaji Mkuu Mstaafu, Hamid Mahmoud Hamid, Mwenyekiti wa ZEC ametangaza uamuzi huo leo tarehe Alhamisi tarehe 2 Julai 2020.

Baada ya mabadiliko hayo, kwa sasa Zanzibar ina majimbo 50 badala ya 54 ilivyokuwa awali, ambapo Unguja ina majimbo 32 na Pemba 18.