Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Dodoma
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo imezitaka ofisi za Umma kutoa taarifa kwa wanahabari kwa kuwa
siyo hisani na siyo hiyari, bali ni takwa la kisheria kwa mujibu wa
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 18 (d).
Michezo imezitaka ofisi za Umma kutoa taarifa kwa wanahabari kwa kuwa
siyo hisani na siyo hiyari, bali ni takwa la kisheria kwa mujibu wa
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 18 (d).
Kauli hiyo
imetolewa na Waziri mwenye dhamana ya tasnia ya Habari Dkt. Harrison
Mwakyembe alipokutana na ujumbe wa viongozi wa Chama cha Waandishi wa
Habari mkoani Arusha (APC), kupitia mradi unaouendesha wa Alternative Media leo jijini Dodoma.
imetolewa na Waziri mwenye dhamana ya tasnia ya Habari Dkt. Harrison
Mwakyembe alipokutana na ujumbe wa viongozi wa Chama cha Waandishi wa
Habari mkoani Arusha (APC), kupitia mradi unaouendesha wa Alternative Media leo jijini Dodoma.
“Serikali haina ugomvi na vyombo vya
habari, bila vyombo vya habari hatutaweza kuwahabarisha wananachi
masuala mbalimbali ya maendeleo ya nchi yetu” amesema Dkt. Mwakyembe.
habari, bila vyombo vya habari hatutaweza kuwahabarisha wananachi
masuala mbalimbali ya maendeleo ya nchi yetu” amesema Dkt. Mwakyembe.
Aidha, amewakumbusha wanahabari kuwa kazi
wanayofanya ni muhimu sana ambapo nchi zilizoendelea bado wanatumia
vyombo vyao vya habari ikiwemo Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC)
ambalo lina miaka zaidi ya 90 na linatangaza habari zake kwa lugha zaidi
ya 40 ili kuwafikia wananchi wake na dunia kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha
Waandishi wa Habari kutoka mkoa wa Arusha Bw. Claud Gwandu amemshukuru
Waziri Dkt. Mwakyembe kwa mapokezi, majadiliano yenye tija kwa uwazi na
ukweli na kumpongeza kwa kazi nzuri anayofanya katika sekta
anazozisimamia.
Waandishi wa Habari kutoka mkoa wa Arusha Bw. Claud Gwandu amemshukuru
Waziri Dkt. Mwakyembe kwa mapokezi, majadiliano yenye tija kwa uwazi na
ukweli na kumpongeza kwa kazi nzuri anayofanya katika sekta
anazozisimamia.
“Tunamshukuru Waziri kwa kutupa nafasi
ili tuweze kushirikiana katika kuimarisha tasnia ya habari iwe bora kwa
mustakabali wa nchi yetu” amesema Gwandu.
Amesema APC kupitia mradi wa Alternative Media imefanya utafiti na kupata maoni ya wanahabari na wadau nchini ambao kwa pamoja wanaiomba Serikali ibadilishe sheria na kanuni mbalimbali ambazo zimekuwa vikwazo vikubwa katika tasnia ya habari nchini ikiwemo kanuni namba 4 ya maudhui mtandaoni inayotaka kila anayeanzisha chombo cha habari mtandaoni (online media), kulipa kiasi cha Tsh1100,000 fedha ambazo ni nyingi kulingana na uwezo wa wanahabari nchini.
ili tuweze kushirikiana katika kuimarisha tasnia ya habari iwe bora kwa
mustakabali wa nchi yetu” amesema Gwandu.
Amesema APC kupitia mradi wa Alternative Media imefanya utafiti na kupata maoni ya wanahabari na wadau nchini ambao kwa pamoja wanaiomba Serikali ibadilishe sheria na kanuni mbalimbali ambazo zimekuwa vikwazo vikubwa katika tasnia ya habari nchini ikiwemo kanuni namba 4 ya maudhui mtandaoni inayotaka kila anayeanzisha chombo cha habari mtandaoni (online media), kulipa kiasi cha Tsh1100,000 fedha ambazo ni nyingi kulingana na uwezo wa wanahabari nchini.
Aidha, Mwenyekiti huyo amempongeza Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kazi
kubwa anayofanya kwa kutekeleza miradi mingi kwa manufaa ya Watanzania
na kusisitiza kwa mwenye macho haambiwi tazama.
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli kwa kazi
kubwa anayofanya kwa kutekeleza miradi mingi kwa manufaa ya Watanzania
na kusisitiza kwa mwenye macho haambiwi tazama.