
EMMANUEL MBATILO
Mwanariadha kutoka nchini Kenya
mwenye asilia ya Longido nchini Tanzania Eliud Kipchoge amekuwa mwanariadha wa kwanza duniani kutumia chini ya
saa 2 kumaliza mbio za marathon (Kilomita 42).
mwenye asilia ya Longido nchini Tanzania Eliud Kipchoge amekuwa mwanariadha wa kwanza duniani kutumia chini ya
saa 2 kumaliza mbio za marathon (Kilomita 42).
Mwanariadha huyo ametimiza ndoto
yake na kuweka rekodi mpya ya dunia leo nchini Austria akitumia saa 1,
dakika 59 na sekunde 40.2 (1:59:40.2) kwenye mashindano maalum ya INEOS
1:59 Challenge.
yake na kuweka rekodi mpya ya dunia leo nchini Austria akitumia saa 1,
dakika 59 na sekunde 40.2 (1:59:40.2) kwenye mashindano maalum ya INEOS
1:59 Challenge.
Kipchoge amevunja rekodi yake binafsi ya kutumia saa 2:01::39 aliyoiweka mwaka jana kwenye Marathon ya Berlin.
Tanzania inajivunia mwanariadha huyu kutokana na umahiri wake wa kukimbia katika ukanda wa Afrika Mashariki.