Mkurugenzi mkuu wa ewura atembelea banda la ewura maonesho ya utalii ya karibu kusini

Mkurugenzi  mkuu  wa  EWURA  Mhandisi  Modestus Lumato katikati akiwa na  wadau na  wafanyakazi wa EWURA alipotembelea  viwanja  vya  maonesho  ya  utalii ya karibu  kusini katika eneo la  Kihesa  Kilolo mjini Iringa leo 


MkurugenziMkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Mhandisi Modestus Martin Lumato amesema  jitihada    zinazofanywa na  serikali ya  awamu ya   sita  chini ya  Rais Samia  Suluhu  Hassa  katika  ukuzaji  wa  uchumi  wa Taifa  kupitia  sekta ya  utalii  ni  kubwa sana  na  wao kama   EWURA wanaendelea  kuunga mkono  jitihada   hizo  kwa  kuhakikisha  wanasimamia  vema huduma  za Nishati na maji  kuona  hakuna  uchakachuaji .

Akizungumza  leo  baada ya  kutembelea  banda la  EWURA  katika  maonesha  ya  utalii ya Karibu  kusini katika  viwanja za  Kihesa Kilolo  mjini  Iringa Mhandisi  Lumato alisema  kuwa  kila mmoja  ni  shahidi kwa kazi nzuri   na kubwa  inayofanywa na mheshimiwa  Rais  Samia  katika  kutangaza utalii  kupitia filam ya The Royal Tour ambayo  imeweza   kutangaza utalii Dunia nzima .


Kwani  alisema  kuwa  wakati  Rais  Samia  akifanya  jitihada  kubwa za  kutangaza  utalii  ngazi ya kimataifa  mikoa nayo  imeendelea  kuunga mkono  jitihada  hizo kama  ambavyo mikoa 10 ya kusini na nyanda za  juu kusini  ilivyoweza  kuandaa maonesho hayo kwa  ajili ya kutangaza  vivutio  vya utalii vilivyopo  mikoa ya kusini na nyanda  za  juu  kusini .


Alisema  mkakati huo  ni mzuri na  utasaidia  kuhamasisha  jamii kupenda  kutembelea  vivutio  vya utalii pia  kuendelea  kufungua  milango kwa  wageni  kutembelea  hifadhi  mbali mbali nchini na kukuza  uchumi wa Taifa .


Mhandisi  Lumato  alisema  wao kama  EWURA kwa  kuunga mkono maonesho ya  utalii ya karibu  kusini  wamechangia  kiasi cha Tsh milioni 10 pamoja na  kuungana na uongozi wa  mkoa wa Iringa na mikoa mbali mbali kwenda  kutembelea   hifadhi ya  Taifa ya  Ruaha .


” Sisi  EWURA   tumeona  ni  juhudi nzuri  katika  kuunga mkono jitihada za  serikali ya  awamu ya sita katika  kutangaza  utalii na wote  ambao  watakwenda kutalii   Hifadhi ya  Ruaha baada ya  kurejea   itakuwa ni mwanzo  wa  kuendelea  kueneza  elimu ya  utalii wa ndani ndani ya  familia na nje ya familia  zao”

Alisema  kuwa  sekta ya utalii  imekuwa  zaidi katika  mikoa ya kasikazin ila  kutokana na  jitihada za  serikali  kutangaza  utalii  nje itasaidia  zaidi  milango ya  utalii kwa mikoa ya kusini  kuongezeka  zaidi.

 Mhandisi  Lumato alisema  kuwa  EWURA  wamekuwa sehemu ya utalii kutokana na  wateja wao ni  watumiaji wa Nishati na maji   hivyo  kupitia maonesho  hayo  wataweza  kutoa  elimu  mbali mbali  kwa wananchi  pamoja na  kupokea  malalamiko yao  kwa  wateja  wa  huduma za  umeme na Maji .

Aidha  alisema  EWURA katika  kuhakikisha  wanaendelea  kutoa  huduma  bora  wataendelea  kuchunguza  ubora wa mafuta pamoja na bei  zao  na  kuona  vituo vya kuuza mafuta  vinakuwa  bora  zaidi na sio  bora  vituo .

Kwa  upande  wao wananchi  waliotembelea   banda la EWURA wamepongeza  jitihada za  EWURA katika  kusimamia ubora  wa Nishati na Maji na  kuwa wanaomba  huduma   hiyo ya  elimu  kwa  umma kuendelea  zaidi .

Banda  la  EWURA  katika  viwanja  vya maonesho ya  utalii  karibu kusini 

Mkurugenzi  mkuu  wa  EWURA  Mhandisi  Modestus Lumato  akiwa katika  banda la Tanesco