MGOMBEA UBUNGE CHADEMA ARUMERU MAGHARIBI AWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE KAMPENI KUSIKILIZA SERA

WANANCHI wametakiwa kuhudhuria kwenye mikutano mbalimbali ya kampeni za kugombea nafasi za kisiasa kuelekea kilele cha uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu ili waweze kuwapima wagombea kwa sera zao.

Hayo na yameelezwa na mgombea ubunge jimbo la arumeru magharibi, Gibson ole Meseiyeki wakati akiongea na wananchi wa jimbo hilo waliohudhuria ufunguzi wa kampeni za ubunge  wa jimbo hilo mapema jana katika ofisi za  jimbo hilo

Gibson alisema kuwa kwa sasa wapo baadhi ya wananchi ambao mara nyingi wanalalamikia wagombea kuwa hawajatekeleza ahadi wakati ahadi hizo hazikuadiwa 

Alisema kuwa mwananchi  anapohudhuria ni raisi sana kuweza kunukuu ahadi za mgombea na kisha kuzifuatilia tofauti na pale wanapokaa majumbani 

Aliendelea kwa kusema kuwa kwa msimu huu ambao kuna kampeni kila mwananchi anatakiwa kuhudhuria na kutafakari hoja za mgombea 

Katika hatua nyingine alisema kuwa yeye kama mgombea ubunge kwa jimbo la Arumeru Magharibi amejipanga kupita kwa wananchi na kisha kuwaeleza kile walichokifanya kwa kipindi cha miaka mitano.

“Kwa kipindi cha miaka 5 iliyopita tumetekeleza miradi mbalimbali ambayo iligusa maisha ya wananchi wa jimbo hili tutaileza kwa kina” aliongeza