Man united yalazimishwa sare 1-1 ugenini na wolverhampton wanderers epl

Mkwaju wa penalti uliopigwa na Paul Pogba ukienda juu baada ya kuokolewa na kipa Rui Patricio dakika ya 68 Manchester United ikitoa sare ya 1-1 na wenyeji, Wolverhampton Wanderers katika mchezo wa Ligi Kuu ya England, Uwanja wa Molineux, West Midlands. Penalti hiyo ilitolewa baada ya yeye mwenyewe, Pogba kuangushwa na  Conor Coady kwenye boksi katika mchezo ambao Man United walitangulia kwa bao la A. Martial dakika ya 27 kabla ya Ruben Neves kuisawazishia Wolves dakika ya 55