Rc makonda ataja anakotoa pesa za kutoa misaada kwa watu

Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema kuwa pesa ambazo huwa
anaonekana akizigawa ni pesa ambazo anazipata kwa wadau na marafiki zake
wa karibu ambao wako tayari kumuunga mkono katika masuala ya maendeleo.





Makonda
ameyabainisha hayo leo Septemba 18, alipokuwa akizungumza mbele ya
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, walipokuwa wametembelea Taasisi ya Moyo ya
Jakaya Kikwete ili kujionea utendaji kazi wa Taasisi hiyo na kupokea
taarifa ya watoto ambao wamekwishapatiwa matibabu, kutokana na utaratibu
wake aliouweka wa kusaidia watoto 10 kila mwezi.

“Mheshimiwa
waziri (Ummy) kuna watu wanasema huyu Makonda anatoa wapi  hela, kwa
mfano zile fedha milioni 10 za Juma Kaseja zimepigiwa kelele
kwelikweli..ooh kapiga penati kapewa milioni 10.



“Jamani
nchi hii ni tajiri na watu wa nchi hii ni tajiri pia, inahitajika tu
mtu mwaminifu mwadilifu anayeomba pesa kwa matumizi sahihi na watu wao
wanatoa pesa. Balozi huyu wa Falme za Kiarabu yupo ana marafiki wengi
lakini huwa namuona wengine wanakunywa naye kahawa basi….” amesema





Aidha
Makonda yupo katika mchakato wa kuunda kamati maalumu ya kufunga mwaka,
yenye mlengo wa kukusanya kiasi cha Shilingi Bilioni 1, kutoka katika
makampuni mbalimbali, fedha zitakazosaidia kuokoa maisha ya watoto wenye
matatizo ya moyo.