Mwanamke mbaroni kwa kumlazimisha mtoto wa miaka8 kufanya nae ngono

Na Mwandishi Wetu, Iringa 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa linamshikilia mwanamke mwenye umri wa miaka 56 mkazi wa Kijiji cha Lumuli – Manispaa ya Iringa, kwa tuhuma za kulazimisha kufanya mapenzi na mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 8.

Mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa Darasa la Tatu amemsababishia michubuko na maumivu sehemu za siri.

Kamanda polisi mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi amesema mama huyo alimvitia mtoto huyo kichakani na kulazimisha afanye naye mapenzi kwa nguvu.