Ndege ya ukraine yaanguka iran ikiwa na abiria 180

Ndege ya Ukraine aina ya Boeing-737 iliyokuwa na abiria 180 imeanguka Iran, kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo.


Ndege
hiyo inayomilikiwa na shirika la kimataifa la ndege la Ukraine
ilianguka muda mfupi baada ya kuanza safari katika uwanja wa ndege wa
Imam Khomeini mjini Tehran.

Ripoti za awali zinadai kuwa ndege hiyo ilikuwa safarini kuelekea mji mkuu wa Ukraine, Kyiv.

Haijabainika ikiwa ajali hiyo ina uhusiano wowote na mzozo wa Iran-na Marekani.

Kikosi cha uokoaji tayari kimetumwa katika eneo la tukio karibu na uwanja wa ndege, eneo ambalo ndege lilianguka