Pprof Helene Carabin kutoka nchini Canada akitoa mada katika mkutano huo |
Minyoo ya Tegu ya Nguruwe (cysticercodis)imekuwa tishio kwa walaji wa nyama ya mnyama huyo na kupelekea kusababisha maradhi mengi kwa binadamu ikiwemo ugonjwa Wa kifafa.
Hayo yamebainishwa na Naibu Wa afya Dkt. Faustin Ndugulile wakati akifungua mkutano Wa kwanza Wa kimataifa Wa kujadili minyoo ya Tegu Wa nguruwe katika thana ya Afya ya pamoja unaofanyika katika ukumbi Wa Mounti Meru Arusha
Mkutano huo umefanyika Leo November 26 ambapo alisema kuwa kwa wale walaji Wa Nyama ya Nguruwe kunaminyoo ambayo iko katika nyama huyo kupitia mayai yanayopatikana ndani ya inaweza kumuathiri binadamu endapo atakula nyama ambayo ijapikwa vizuri pamoja na mbogamboga ambazo azijaoshwa pamoja nakupikwa vizuri.
Alisema athari zinazoweza kupatikana katika mnyama huyu ni kubwa ikiwemo kupata ugonjwa Wa kifafa , na tatizo hili limeshaingia katika nchi yetu na limeanza kuathiri zaidi katika mikoa ya Manyara, Njombe, Mbeya ,Sogwe ,Mbeya pamoja na mkoa Wa Arusha na asilimia 16%ya wananchi wanaoishi mikoa hii wameshaathirika na ugonjwa huu.
“Lengo kubwa kuweka mkakati Wa pamoja Wa jinsi gani tunaweza kutokomeza ugonjwa huu Wa minyoo Wa Tegu Wa Nguruwe,nanianze kutoa rai kwa wafugaji Wa Nguruwe kufuga kisasa na kuacha wanyama wao kuzurura hovyohovyo kwani anavyozurura ovyo anaeza kuacha kinyesi chenye mdudu huyo katika mboga.
” alisema
Alibainisha kuwa hadi sasa serikali yetu haijapata chanjo kwa ajili ya kumzuia mnyoo huyo wa nguruwe na ipo katika utafiti wakuangalia namna ya kumthibiti,lakini pia tunaweza kuzuia kwa kuakikisha kuwa tunafuga bila mifugo yetu kuzagaa,pia kwa wale tunaochinja tuhakikishe tumewapima mifugo yetu kwanza bila ya kuwachinja
Kwa upande wake mkuregenzi mkuu wa Taasisi ya magonjwa ya binadamu (NIMR)Prof Yunus Mgaya wanatekeleza mradi huu kwa kusanya taarifa za kutosha kuhusiana na minyoo huyu wa Tegu ambaye anapatikana kwa kula mbogomboga ambazo zimebeba mayai yaliotokana na vinyesi vya nguruwe au kinyesi cha binadamu
“mradi huu unatekelezwa na nchi zingine mbili Afrika ambazo ni Msumbiji pamoja Zambia na tunashirikiana na wadau wetu wa utafiti wa ujerumani kutoka chuo kikuu cha Munchen ,mradi huu umetuwezesha kununua vifaa vya maabara kwa ajili ya kuweza kufanya utafiti wetu vizuri kwa kiwangoncha juu ,pia umetusaidia kuwapeleka vijana wetu kwenda kupata elimu katika shahada zauthamini PHD, lakini mradi huu umetuleta pamoja nchi hizi za Afrika na lengo kubwa ikiwa ni kutokomeza au kuzuia watu wasipate ugonjwa huu unaotokana na minyoo hii ya Tegu ”
Naye Kaimu mkuu wa idara ya tiba ya mifugo na afya ya jamii ambaye pia ni mkurugenzi wa mtandao wa utafiti wa kisayansi Prof,Helena Ngowi alisema kuwa mnyoo ni hatari sana kwa sababu anaweza kuleta adhari kubwa katika utumbo wa binadamu hadi katika ubongo wa binadamu.